KAMA UNA MBAVU ZA AKIBA-SOMA HAPA

Jamaa alionekana kapona hivyo atolewe kwenye hospitali ya machizi arudishwe kwao. Asubuhi mmoja akachukuliwa na ambulance mpaka jirani na kwake, akaulizwa unapafahamu hapa? Akajibu ' Ndio nyumba yangu ileee". Ghafla mlango wa nyumba ile ukafunguka wakatoka watoto wawili wamevaa yunifom,'Hee na watoto wangu walee wanaenda shule'. Mara akatoka mwanamke, jamaa akafurahi,' Mke wangu yule, mke wangu jamani'. Madaktari walianza kumfungulia atoke kwenye gari ghafla mwanaume akatoka kwenye ile nyumba, jamaa akaangalia kwa makini kisha akaruka kwa furaha,' Mimi yulee naenda kazini, unaona nilivyopendeza na suti ile nilinunua Mariedo'. haraka sana akarudishwa hospitalini.