MAREHEMU STEV JOBS NA TUZO YA POSTHUMOUS

       Hii ni habari mpya kabisa ambaye imetujia mapema hivi leo kuwa yule muasisi wa bidhaa za apple,Steve Jobs ametunukiwa tuzo ya posthumous ikiwa ni heshima na ishara ya kumkumbuka Mr Jobs kwa mafanikio aliyopata enzi za uhai wake.Pia imepangwa kufanyika kwa maadhimisho maalum tarehe 11 feb,2012 kwa ajili ya heshima yake.ili kusindikiza shughuli hiyo ikiwa ni siku moja kabla ya kurushwa rasm kwa utoaji wa tuzo hizo katika CBS
        Najua wengi watajiuliza kuwa Mr job ambaye alifariki octoba 2011,kwanini amepewa tuzo hizo na yeye hakuwa mwanamuziki,wala produza?
  
 Hii imekuja baada ya mchango mkubwa alioutoa Mr job katika bidhaa zake ambazo nyingi zilikuwa ni za muhimu sana katika suala zima la muziki kama vile ipad,iphone,ipod na apple computers,hivyo watu wengi sasa wanaweza kusikiliza na kufurahia muziki kupitia bidhaa zake hizo.

Comments