JE NI BIFU MPYA KATI YA ALIKIBA NA WIZKID?

Baada ya wizkid kunyang'anywa tuzo aliyopokea siku chahche zilizopita kupitia MTV, ya Best african Act na kupewa Msanii toka Tanzania Alikiba.Ni mwanzo wa bifu lingine kwa mashabiki wa wasanii hao.Kupitia mitandao ya kijamii instagram na tweeter mashabiki wa alikba wamekuwa wakishangilia Ushindi huo huku wakirusha vijembe kwa Mashabiki wa Wizkid na Msanii mwinfgine toka TZ,Diamond platnumz.Vile vile Mashabiki wa Wizkid hawakuwa nyuma katika kujibu vijembe hivyo kwa kusema kuwa,msanii ALikiba hakustahili tuzo hiyo,ila Imekuwa kama Bahati kwake.


Uongozi wa mtv ulifikia maamuzi hayo baada yakugundua kuna makosa yalifanyika katika kuhesabu kura hizo,Hivyo baada ya kufatilia kwa makini waliona kuwa Tuzo hiyo ilikuwa ni halali kwa Alikiba na sio WIzkid kama Walivyotangaza awali.