DIAMOND PLATNUM AHAMIA KWA,ELIZABETH MICHAEL (LULU )???



Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu ambaye ni star mkubwa wa filamu nchini Tanzania anadaiwa kukataa kumvulia nguo Diamond Platinumz anayehaha kutaka kulifaidi penzi lake kiasi cha kufikia hatua ya kumnunulia gari aina ya Nissan Murrano yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 za kitanzania ..

Ili kumaanisha kuwa hataki kutoka kimapenzi na Diamond , Lulu alilazimika kubadili namba yake ya simu ya mkononi ili kuepuka usumbufu kutoka kwa Diamond.... 

Habari za chumbani zinaarifu kuwa, lengo la Diamond kutaka penzi la Lulu ni kutaka kuzidi kutawala vyombo vya habari kwani Lulu ni star mkubwa na mwenye mvuto kwenye media na pia ni mtu mwenye mashabiki wengi.

Diamond anaamini kuwa akiwa na Lulu kimapenzi umaarufu wake utazidi kuongezeka maradufu kwa kuongelewa na watu kila siku lakini Lulu hasikii la muadhini wa la mnadi swala katika hilo na hivi majuzi tu Lulu alitangaza kumzimikia Justin Bieber ili kuzidi kumvunja moyo Diamond

SOURCE    MPEKUZI