UMEISIKIA HII!! MLIMA KILIMANJARO KUOTESHWA MBAWA MWAKA HUU


Wakati asilimia kubwa ya Watanzania wakiwa hawana hili walalile (pengine kutokana na uzembe wa baadhi mamlaka au watu binafsi wenye dhamana kukwepa au kuzembea kutimiza wajibu wao kikamilifu), mamilioni ya watu sehemu zingine duniani wanajiandaa kushuhudia historia ya kipekee kuwahi kutokea duniani, ikiandikwa kutokea katika moja ya miji maarufu ya nchi hii iliyoko katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Tukio hili ambalo litakuwa la kwanza na huenda pia likawa ndio la mwisho kuwahi kutokea, linatarajiwa kujiri Januari 27 ya mwaka huu, ambapo wanaharakati wa masuala ya kijamii wapatao 200 toka sehemu mbalimbali za dunia, watakusanyika katika kilele cha mlima mrefu kuliko yote barani Afrika, Mlima Kilimanjaro, tayari kabisa kwa ajili ya kupaa angani na kuuzunguka mlima huo kwa kutumia myavuli maalum ya kurukia angani, chini ya mradi ambao umepewa jina la Wings Of Kilimanjaro (WOK), ama kwa kiswahili waweza kuuita mradi huo kuwa ni “Mbawa za Kilimanjaro”
Ni tukio ambalo awali liliasisiwa na Adrian McRae, mwanaharakati wa masuala ya kijamii aliye raia wa Australia, ambaye ameeleza kuwa, lengo la kubuni mradi huo lilikuwa ni kuchagiza ukusanyaji wa fedha kwa ajili ya kusaidia jamii zilizo chini ya mlima huo, ambazo zimejawa na uhitaji wa mambo kibao ya kimsingi.

Comments