HII NDIO RIPOTI KUHUSU MVUA KUBWA ILIYOEZUA NYUMBA ZA WATU MTWARA




Mkuu wa wilaya ya Mtwara Wilman Ndile amesema kuwa nyumba 45 zimeezuliwa mapaa ikiwemo shule ya msingi Ligula, shule ya sekondari Marwa Islamic na kanisa la Victoria Ligula









Nyumba 113 zimebomolewa na mvua zinazoendelea kunyesha katika halmashauri ya manispaa ya Mtwara Mikindani na kuacha mamia ya watu wakiwa hawana mahali pa kukaa.Amefafanua watu waliokosa hifadhi wamehifadhiwa kwa muda kwenye madarasa ya shule ya msingi Rahaleo wengi wao wakiwa wamepoteza vitu vyao vyote.






Maeneo yaliyoathiriwa zaidi na mvua hiyo ni Mdenganamadi, Magomeni, Mikindani, Nandope na kiangu ambapo bwawa la Maji machafu la manispaa ya Mtwara limejaa.

Comments