WEMA KAWAPOTEZA WENZAKE MSIBA WA SHARO

Msanii nyota wa filamu nchini na aliyekuwa MissTanzania 2006/07 Wema Isack Sepetu katikati ya wiki iliyopita alilitia aibu kundi la bongo muvi kwa kufanya kitu cha kipekee kwenye msiba wa mwanamuziki na msanii wa komedi aliyefariki kwa ajali Mkoani Tanga Sharo Milionea. Wema Sepetu ambaye siku za hivi karibuni amepumzika skendo kwenye vyombo vya habari alipongezwa na watu kwa uungwana aliounonyesha baada ya kutoa mchango mwingi kuliko msanii yeyote wa kundi hilo linalosifika kwa kashfa za ngono. Habari zilizothibitishwa na mmoja wa ndugu wa marehemu ambae aligoma kutaja jina lake kwa madai kuwa yeye si msemaji wa familia alisema kuwa "Ni kweli wasanii mbalimbali walijitolea kwa kuja huku Tanga lakini Wema ndiye aliyetoa mchango mkubwa sana kwa kutoa shilingi laki mbili peke yake 200,000/= huku wasanii wengine wakiishia kutia aibu” Alisema mtu. Aidha ilidaiwa Wema ndiye aliyeonekana kuwa na uchungu wa dhati toka moyoni ambapo licha ya mchango huo pia alionekana kujishughulisha na kazi za kusaidia majukumu msibani hapo bila kujali ustaa wake aliokuwa nao

Comments