SEAN PAUL KUOA MWEZI HUU

Mkali wa dancehall duniani sean paul ambaye anaendeleakufanya vizuri kupitia songs zake kama she doesnt mind,got to love you na hold you tonight anatarajia kumuoa mchumba wake wa siku nyingi ,Odi ‘Jinx’ Stewart mwezi huu.
Kuhusu siku na tarehe ya tukio hilo bado limekuwa siri kubwa na wasemaji wake wakuu wamekuwa wasiri sana kwani hawataki ishu hiyo kuchuja sana.chanzo chetu cha habari kinasema kuwa wapambaji na wageni wengi wametakiwa kuwa siri mpaka pale itaruhusiwa kutangazwa,
 ''Unajua ulinzi wa kutosha sana unatakiwa unapokuwa unaandaa harusi kama hii ili watu wenye malengo mabaya washindwe kuharibu mipango tuliyojiwekea" alisema mmoja wa wasemaji wa shughuli hiyo 

Comments