
Jamaa mmoja alienda kuomba kazi kwenye ZOO. Akaambiwa nafasi ya kazi ipo
ila hakuna sokwe" hivyo utajifanya sokwe na tutakupa ngozi ya sokwe
utavaa" Jamaa siku ya kwanza akavaa, walipokuja watalii mambo yalienda
vizuri. Siku iliyofuata banda lake liliwekwa kwa juu ya banda la simba.
Jamaa ktk kuongeza mbwembwe akawa anarukaruka, kwa bahati mbayasi
akaangukia ndani ya banda la simba. Akawa anapiga kelele "mama nakufaa!"
Mara yule simba akamwambia "acha ufala wewe kelele za nini sasa, mimi
mwenyewe binadam!, rudi kwenye banda lako kabla watalii hawajaja
watatushtukia.