AMCHOMA MWANAMKE MWENZAKE PASI YA MAPAJANI KISA N1000/=


Mwanamke mmoja Nchini Nigeria amekamatwa na polisi na kufunguliwa mastaka baada ya kumuunguza mtoto  wa miaka 15 aliyekuwa anamsaidia kuuza katika duka lakela nguo, kwa pasi yenye moto mapajanani na kumsababishia majeraha makubwa kwa kile iliyochodaiwa kupotea kwa hela yake yenye thamani ya naila 1000 katika duka lake alilokuwa anafanyia biashara(wataalamu wa kubadili mtakuwa mnajua ni shilingi ngapi kwa kitanzania)

Mwanamke huyo Kudirat Isekolowo anayeishi Igbehinadun alijitetea kuwa hakuwa akijielewa wakati anafanya kitendo hicho hivyo ilikuwa ni hali ya kutokutegemea(out of control)

Mtoto huyo aliondoka nyumbani kwa wazazi wake na kupelekwa kwa Isekolowo kwa lengo la kumsaidia kazi ndogondogo dukani hapo na ameanza kuishi nae tangu Novemba 2012.Lakini ndipo bila kutegemea alijikuta akipewa majeraha hayo makubwa ambayo hayawezi kufutika mwilini mwake yaliyowaliza baadhi ya wafanyabiashara waliokuwa karibu na duka la mwananke huyo ambao waliona tukio hilo

Comments