JINSI WEMA SEPETU ALIVYOKUTANA NA KANUMBA SIKU YA KWANZA






Nakumbuka nilipokutana na marehemu nilikuwa niko na dada yangu mimi nilikuwa nakaa na dada yangu, kwasababu once nilishawahi kuishi na mama yangu and then from there unajua baada ya kuingia kwenye nini nini nikawa busy. Dada yangu mimi kaolewa lakini kwa dada yangu nilikawa nahisi kama pako free zaidi, kwamba mama ukirudi ‘umetoka wapi sijui nini na nini hivyo, alikuwa haelewi. So ikabidi tu nianze kuishi na dada yangu. Kwahiyo dada yangu akawa ananielewa, kwasababu hayupo sana protective kama mama. Siku hiyo tunabadilisha seating arrangement ya pale nyumbani kwa dada yangu tukawa tunatafuta carpet like different furnitures, so tukawa tumeenda hapa kulikuwa na hili duka kubwa hivi la Mwanamboka kulikuwa kuna furniture center, Pentagon, so tukawa tumeenda pale wakati tunaenda tulimkuta Kanumba wapo nje wameweka makamera yao nini ,wanashoot Lost Twins. So sisi tumeingia tunaona tu makamera, tumepark gari tumeingia ndani tunaangalia furniture. Akatokea Maya tukasalimiana akaniambia, ‘ jamani nakupenda’ na mimi nikamwambia na mimi napenda unavyoigiza’ nini na nini. 
Tukatoka nje tukakutana tena na Maya akaniambia ‘jamani jamani kama unaweza pita kidogo tu hata uonekane, hata usalimie’. Nikamwambia siwezi kwasababu nipo kwenye mkataba, akina Uncle Hashimu wataniua wakiniona nimefanya kazi au nimetokea kwenye nini bila kuwaconsult so akaniambia ‘basi sawa tuachie namba yako’. Wakati ananiambia tuachie nambo yako, Kanumba huyo anapita, ‘Kaka kaka ngoja umemuona Wema?’ Aliniringia sana. ‘Mambo’ nikamwambia ‘fresh vipi’ ‘safi’ nikamwambia poa,’Kaka basi chukua namba yake ya simu tunaweza baadaye like tunaweza tukamtumia kwenye movies’, ,Kanumba akamwambia achukue simu yake ndani. 
Basi nikamwangalia mimi mwenyewe basi ndio ninamwona mara ya kwanza, ‘Hee Kanumba’, kwasababu nimeangalia sana michezo yao. Basi, so baada ya hapo akaleta akachukua namba yangu akanibeep nikamsave, basi mimi nikaondoka zangu. Sijafika mbali naona namba inanipigia ambayo nimeisave vilevile Steven Kanumba, nikapokea ‘Hello’ akaniambia ‘vipi, safi Kanumba hapa’ nikamwambia ‘namba yako nimeisave’ ‘haya basi sawa basi baadae’ nikamwambia ‘poa’. Mara like jioni jioni hivi akaanza kunitext ‘mambo’ ‘Safi’ ‘vipi uko wapi?. Basi kila siku tukawa tumejengeana tabia ya kutextiana kila siku tunandelea for one weak tunatext mara yeye ataniuliza umekula nini, mara sijui nini, obvious kwa mwanamke unakua tu unajua kwamba mwanaume akiwa ana interest na wewe. 
 
Kidogo tukaanza kuulizana una boyfriend una girlfriend sijui nini, hivyo. Akaniambia mimi ‘nipo kambini Lamada’ akanielekeza nikafika. Basi nimefika siku hiyo tumekaa pale garden akaniambia ananipenda na nini, hivyo. Kipindi hicho nilikuwa sina boyfriend nilikuwa very very single, so nikamdanganya nikamwambia ‘mimi na boyfriend wangu sijui nini’ akaniambia ‘naomba tu just like nifikirie basi’ Nakumbuka tulivyokuwa tunaondoka ndo tukakiss, it was our first kiss. Basi nikaondoka, akaniambia ‘unaweza kurudi tena nikamwambia siwezi akaniambia please, please naomba urudi tena unikiss’ nikamwambia ‘sawa’ basi nikarudi then akaniambia ‘l love you, love you too, mapenzi yakaanza. Basi kwenye mapenzi yetu ndo akaniambia like ‘nataka kuact movies na wewe’ nikamwambia ‘mimi siwezi kuact’ akaniambia ‘mimi nahisi unaweza kuact hujajua tu’ nikamwabia sijawai kufikiria kuact, akaniambia ‘unaweza kulia’, nikamwambia ‘nilie nina sababu gani ya kulia’ akaniambia ‘basi kama huwezi kulia tutakumenyea vitunguu, ‘vitunguu ukimenya si unalia, basi tutakuwa tuna kumenyea vitunguu’ . Akaniambia niende kuonana na bosi wake. Nilivyofika tu ofisini nikaonana na Mtitu Game. Akanipa script akaniambia nikasome kama story akaniambia ‘wakati unasoma uwe unasoma sana concentrate kwenye Dina.
 Basi vile tukiwa tukikutana tunafanya mazoezi nini, akaniambia ‘sawa basi wewe you are ready to shoot. Nilivyo shoot movie yangu kwanza, hauwezi amini, I just felt yaani kwanza niliona iko very easy. Kwa wengine wanaona it’s hard unajua. Baada ya hapo ndo nilikuwa tayari nimetoa taji, I had to go back to school. Nikasafiri nikaelekea Malaysia kufanya kozi yangu ya mwaka ya International Business, wakati niko Malaysia nikatumiwa movie yangu ya Point of No Return. Tumekaa tunaangalia na marafiki zangu nikaona kwamba kumbe it’s nice, it’s fun. Nikampigia simu, ‘narudi for likizo soon naomba uniandalie script nataka ni shoot movie nyingine’ Nimerudi kweli ndo tukashoot Red Valentine, Family Tears, White Maria yaani tukashoot movie movie nyingi hivi so from there nikawa nimeshajikuta katika movie, so that why I keep saying kwamba without him nisingejua.

haya ameyasema yeye mwenyewe alipofanya mahojiano na mtandao flan hapa nchini

0 comments: