TSH 1000/= ILIVYOTOA UHAI WA BONDIA MASHALI

Ikiwa bado watanzania wapenda ndondi wakiwa na msiba mzito wa Bondia Thomas Mashali,Aliyefariki dunia mapema wiki hii kwa kupigwa na watu wasiofahamika.Taarifa iliyopatikana toka kwa Mtoto wa marehemu inasema kuwa,kulitokea kutoelewana kati ya Dereva bodaboda na Marehemu mashali,Ambapo marehemu alikodi bodaboda impeleke mahali akijua kuwa gharama ni Tsh 2000/= laikini baada ya kufika dereva bodaboda akasema kuwa Gharama ni tsh 3000/=,ndipo mabishano yalipoanza.na kepelekea ugomvi.

Baada ya kuona anaelemewa,Dereva boda boda akaanza kuita kelele za mwizi ndipo wananchi walipoanza kumshambulia Marehemu mashali,Ambaye alifariki muda mfupi baada yakufika hospitalini.Thomas Mashali alifariki dunia usiku wa kuamkia October 31, 2016 na amezikwa November 2, 2016 kwenye makaburi ya Kinondoni Dar es salaam.