BAADA YA MIAKA 30 MBELE DINI INAWEZA KUPOTEA KABISA

 
Utafiti kuhusu imani ya watu wanaoishi katika nchini 137 ambao umetengeneza kitabu chake kipya, umegundua kuwa upagani unazidi kuongezeka zaidi kwenye nchi zilizoendelea kutokana na utajiri.
Utafiti huo umeelezea pia imani maarufu kuwa watu wenye dini watawatawala wapagani kwakuwa wao (watu wa dini) huzaa watoto wengi.
Dr Nigel Barber amekiita kitabu chake, ‘Why atheism will replace religion,’ (Kwanini upagani utachukua nafasi ya dini).
Amesema wapagani wengi wapo kwenye nchi zilizoendelea kiuchumi na dini itapungua kwa watu kutokana na kuongezeka kwa utajiri wa mtu mmoja mmoja.