CHEKA NA NASMILE !!! HAKIKISHA UNA MBAVU ZA KUTOSHA




MTOTO: Baba ntumie hela ya matumizi huku shuleni hali ni mbaya la sivyo ntajinyonga. BABA:huku nyumbani hali ni mbaya kuliko huko shuleni kwahiyo kama unajinyonga sawa tu kwa sababu utapunguza bajeti. Kopa kamba dukani nitakuja kulipa nitakapokuja kuchukuwa mwili. Mungu akulaze mahali pema pepon
.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
mume anaingia ndani kutoka kazini na kusema."mke wangu nina matatizo makubwa" "sema tuna matatizo mume wangu sisi tu mwili mmoja" mke anapoza "ok! tuna matatizo mke wangu, tumempa mimba secretary wetu" mume anasema.
.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Jamani hapa duniani kuna watu wana mambo ya ajabu, juzi nikiwa kanisani nilikaa karibu na kijana mmoja. Kijana huyu badala ya kusikiliza mahubiri yaliyokuwa yanatolewa na Padri pale kanisani akachukua sigara yake akawa anavuta pale pale alipoketi. Kwa kweli nilishituka nikataka kudondosha chupa yangu ya bia. Nilishangaa sana.
,............................................................................
 Kiswahili cha Mkurya!
Ndugu sangu tumekucha hapa maarum kwa chambo moja tu. Mama Chacha kafirwa na kaka yake usiku wa kuamkia reo. Chambo ra kufirwa si chambo ra mcheso, ukifirwa unaumia sana na chambo hiri sio ra mtu mmocha tu, reo kafirwa Mama Chacha, kesho nitafirwa mimi, keshokutwa utafirwa wewe. Yaani kira mtu razima afirwe tu!
.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Ilitokea ajali ya barabarani lakini kwa bahati nzuri abiria walipata mikwaruzo tu kidogo isipokuwa mmoja ambaye alifariki hapo hapo. Katika walioumia, mmoja aliyekwaruzika mguu na kutoka damu nyingi, alikuwa analia kwa kelele. Baada ya kuona kelele zimezidi, abiria mmoja alishindwa kustahamili na kumkabili yule majeruhi. "Wewe ha**thi nini? Kelele tu! Yo yo yo, uwii uwii uwii! Mwangalie mwenzako yule pale, amekufa na yuko kimya, wewe kwa kuumia mguu tu kelele hatuna amani. Pumbafff!!!"
,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.,.
mzee mmoja alichoshwa na habari za mtaani kwamba mwanaye hata umuulize swali jepesi kupita yote ni lazima atakosa !!! Siku moja akaamua kuandaa swali jepesi kupita kiasi ili amuulize mwanae mbele ya watu kufuta ile historia mbaya !!! Siku ya siku ikafika mbele ya umati mshua akamuita mwanae kisha akamuuliza swali lifuatalo..... mwanangu mtu mwenye umri wa miaka kati ya 18 hadi 35 huitwa KIJANA..... Je mtu mwenye umri kuanzia 36 hadi 50 ataitwa nani !..... Toto bila hata ya kufikili kwa sauti likajb ANAITWA KIJUZI !!!! Vp angekuwa mwanao ungemfanyaje !.
.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Ukiona matatizo yamekuzidi,jaribu kuimba,utagundua kuwa sauti yako inamatatizo kuliko ata uliyonayo.....