HIZI NDIO PICHA ZA MAANDAMANO YA WANAFUNZI WA IFM KWA KAMANDA KOVA!!! @9photoss


Kufuatia wimbi la majambazi kuwasumbua na kuwafanyia vitendo vibaya ikiwemo kubakwa kwa wanachuo hao,wameamua kuandamana mpaka katika ofisi za makao makuu ya polisi na kutaka kuongea na Kamanda wa Polisi wa Kanda maalum ya Kipolisi ya jiji la Dar es Salaam Suleiman Kova ili atoe tamko kwanini ombi lao la kuomba ulinzi katika hostel zao hizo zilizopo kigamboni kutofanyiwa kazi na matokeo yake kila siku wanazidi kufanyiwa vitendo vya kinyama na majambazi.

Wanafunzi hao walidai siku ya Ijumaa walifanya kikao na jeshi hilo ili wawape ulinzi lakini suala la ajabu siku waliyofanya kikao na Jeshi hilo ndio siku waliovamiwa wenzao wawili wakiume na kubakwa  hali iliyosababishwa wanafunzi hao kubakwa. Majambazi hao wamekua wakidai kupewa Laptop simu na fedha kama mwanafunzi akikataa humfanyia vitendo vya kulawiti.

Comments