RAIS KIKWETE KUWAPA POLE WAJANGA WA AJALI YA MELI ZANZIBAR





Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Jakaya Kikwete.amefika nchini zanzibar kwa ajili ya kutoa pole kutokana na ajali ya  meli ya MV Skagit iliyopata ajali visiwani Zanzibar, iliyoondoka Bandari ya Dar es Salaam saa 06.05 mchana juzi ikiwa na abiria 248, watoto 31 pamoja na mabaharia 9.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete walitembelea Uwanja wa Maisara, Zanzibar, ambako ndiko miili ya marehemu huletwa kwa utambuzi na hospitali kuu ya Mnazi Mmoja 

meli ya mv skagit ikimalizia kuzama
Meli hiyo inayomilikiwa na Kampuni ya Seagul Transport, ilipata usajili katika Mamlaka ya usafiri  Bandari Zanzibar (ZMA)ikiwa na uzito wa meli (GRT)96.
Idadi ya watu waliopoteza maisha hadi sasa ni zaidi ya 34, majeruhi 146 wakati wengine wakiendelea kutafutwa.

Zoezi la uokoaji linaendelea katika eneo la tukio kwa msaada wa Mv Flying Horse, Mv Kilimanjaro 111, Tug Bandari ya Zanzibar, KMKM, Mv Zanzibar 1, Polisi wa majini, pamoja na Navy, hata hivyo bado taarifa sahihi za waliopoteza maisha hazijapatikana kulingana na watu hao kuokolewa katika mazingira tofauti



 

Comments