IMEGUNDULIKA!!! KWANINI WANAWAKE WANATOKA NJE YA NDOA?

Karibu katika blog hii pendwa nchini ambayo inakuletea habari mbalimbali za burudani,michezo na jamii bila kusahau mapenzi na urafiki.Leo katika uchunguzi wangu niliokuwa naufanya kimyakimya na kwa umakini mkubwa kuhusiana na kuvunjika kwa ndoa na mahusiano ya wapenzi wengi,nimepata mwangaza  wa sababu kubwa chache ambazo zinasababisha hayo yote.Hata hivyo kwa leo nitaanza na sababu ambazo zinawababisha wanawake kutoka nje ya ndoa.

KWANZA  kabisa ambacho wanawake wengi  wanapatwa na mpondeko wa moyo pale wanapokaripiwa na  mara kwa mara, kukosolewa mbele za watu, au kubughudhiwa. hiii haina ubishi hata kidogo kuwa wanaume wengi wamekuwa ni watemi kwa wapenzi wao.Hapa naomba tubadilike wnaume wenzangu mwanamke hapigwi ila anabembelwa kwa  upole na upendo atakuelewa tu.UKIWAPIGA au KUWATESA wanaamua kutoka nje ya ndoa ili kutafuta faraja pamoja na kujisahaulisha kwa muda, majuto yao kwa kuolewa na watu wasiokuwa na mapenzi ya dhati.


PILI ni mwanaume kujisahau au kusahau wajibu wake  kwa mkewe.utakuta mwanzoni ulikuwa unampelekea zawadi tena unawahi kurudi nyumbani na kujumuika pamoja katika chakula na vitu kama hivyo lakini baadae,ghafla hakina tena zawadi,kurudi nyumbani ni saa 8 usiku.tena ukiwa tilalila.wakati mwingine huli nyumbani wala huna mpango wa kumuuliza mwenza wako kuhusu hali yake  kwa ujumla n.k. Mfano wakati wa uchumba mwanaume alionesha kumjali mwanamke lakini baada ya ndoa mwanamke huyo akaambiwa aache kazi ili kupata muda mwingi wa kufanya shughuli za nyumbani.

SABABU NYINGINE NI  Kutoridhishwa kimapenzi; Kuna wanawake wengi wamekuwa hawaridhishwi katika suala zima la tendo la ndoa. Kuna wengine hawajui nini maana ya kuridhishwa kwa namna ambavyo labda wanaume zao hawawajali katika suala hilo.
Ikiwa  mtu huyo aliwahi kuwa na mpenzi ambaye aliwahi kumpa raha, na sasa yuko kwenye ndoa, mume hajali hisia zake, hilo laweza kuwa ni sababu tosha ya mwanamke kutoka nje ya ndoa.

Nini la kufanya?; Ni vizuri wanandoa kujifunza namna ya kutoshelezana. Wanaume wanapaswa kuacha kujipendelea.

PIA mwanaume amekuwa ni mtu wa kuhisi vibaya haraka sana bila hata kuuliza wala kutafiti. Kuna wanaume wengine wamekuwa maarufu sana wa kuhisi…tena  husema mambo hata kama hawana hakika nayo…utasikia wanasema ‘aaah wewe malaya’…ni makosa kusema vitu usivyo na hakika navyo.

Wakati mwingine mtu hata kama alikuwa anakuogopa, na alikuwa anajiheshimu, anapoona kumbe unamtuhumu kwa vitu ambavyo hafanyi, anaweza kuamua kufanya kweli. Acha kumsema mtu kitu ambacho huna uhakika.




SASA KUTOKANA NA SABABU HIZO CHACHE AMBZO NIMEDHIOLODHESHA HAPO NADHANI WANAUME MTAKUWA MNAJUA MAKOSA YENU.SIO UNAKIMBILIA KUSEMA KUWA NINA MKOSI NA WAKATI TATIZO NOI DOGO TU.USIKOSE KATIKA SEHEMU YA PILI AMBAYO ITAKUELEZEA SABABU ZINAZOWAFANYA WANAUME KUTOKA NJE YA NDOA.KAMA UNA CHOCHOTE CHA KUULIZA,USHAURI AU MAWAZO USISITE KUANDIKA HAPO CHINI KATIKA BOZI LA COMMNT AU SMS KWENDA 0719 698 698 NA ITACHAPISHWA

Comments